Bwana Yesu Asifiwe!!
Tunaendelea tena leo kukuletea mfululizo wa nguvu zilizomo na
uwezo uliomo katika Damu ya Yesu Kristo.
Mathayo 27:29 inatuambia ya kuwa Yesu alivikwa “taji ya miiba”
kichwani pake; na “wakamdhihaki, wakisema, salamu, Mfalme wa
Wayahudi”.
Waliomsulubisha walipokuwa wanamdhihaki katika tendo hilo,
hawakujua kwa Damu ya Yesu iliyomwagika wakati huo, ilikuwa
inaandaa mazingira ya watakaomwamini kufanyika wafalme!
Hii ni kwa sababu “taji” ni sehemu ya vazi la kifalme! Ufunuo wa
Yohana 5:9,10 inatuambia ya kuwa juu ya Yesu: “Ukamnunulia
Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na
taifa, ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao
wanamiliki juu ya nchi”.
Tafsiri za biblia za kiingereza zinasema “Ukawafanya wafalme na
makuhani kwa Mungu wetu, nao wanamiliki juu ya nchi”. Kwa hiyo,
kama unamwamini Yesu na umeokoka, umefanyika mfalme katika
Yeye. Je, unalijua hili? Na je, unaliamini kwa kiwango kipi? Je,
unajua kuishi na kutawala kama mfalme katika ulimwengu huu
maana yake nini? (Warumi 5:17).
Tunaendelea tena leo kukuletea mfululizo wa nguvu zilizomo na
uwezo uliomo katika Damu ya Yesu Kristo.
Mathayo 27:29 inatuambia ya kuwa Yesu alivikwa “taji ya miiba”
kichwani pake; na “wakamdhihaki, wakisema, salamu, Mfalme wa
Wayahudi”.
Waliomsulubisha walipokuwa wanamdhihaki katika tendo hilo,
hawakujua kwa Damu ya Yesu iliyomwagika wakati huo, ilikuwa
inaandaa mazingira ya watakaomwamini kufanyika wafalme!
Hii ni kwa sababu “taji” ni sehemu ya vazi la kifalme! Ufunuo wa
Yohana 5:9,10 inatuambia ya kuwa juu ya Yesu: “Ukamnunulia
Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na
taifa, ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao
wanamiliki juu ya nchi”.
Tafsiri za biblia za kiingereza zinasema “Ukawafanya wafalme na
makuhani kwa Mungu wetu, nao wanamiliki juu ya nchi”. Kwa hiyo,
kama unamwamini Yesu na umeokoka, umefanyika mfalme katika
Yeye. Je, unalijua hili? Na je, unaliamini kwa kiwango kipi? Je,
unajua kuishi na kutawala kama mfalme katika ulimwengu huu
maana yake nini? (Warumi 5:17).
No comments:
Post a Comment